Monday, May 25, 2009

Changamoto katika kujifunza Lugha.

Pengine, ni changamoto kuwasiliana katika lugha nyingine na watu wa utamaduni mwingine. Basi, utuambie kichekesho kuhusu kujifunza kufanya kitu au kusema kitu au kuelewa kitu katika Afrika Mashariki na katika Kiswahili. Chochote ni sawa, lakini ujaribu kutuchekesha! Kwa mfano, nafikiri niliwaambia watu wote kuhusu chakula cha asubuhi ambacho nilipika na sukari nyingi. Familia yangu ya Tanzania ilisema kilikuwa “kitamu sana!” lakini hawakukipenda na sikuelewa kwa sababu nilifikiri “tamu” ilifasiriwa “delicious” tu. Ninatumaini mimi si mtu pekee ambaye nimepata changamoto kama hii. Hebu tuelezee changamoto yako uliyokutana
nayo.

ku*wasiliana -to communicate

ku*fasiriwa -to be translated

Tuesday, May 19, 2009

Ungependa kukutana na nani katika maisha yako na kwa nini?

Ungeweza kukutana na mtu yeyote ambaye yuko hai au amekufa, ungechagua kukutana na nani na kwa nini?

Na Rachel

Tuesday, May 12, 2009

Kwa nini ungependa kuwa mtu maarufu?

Ukiwa na nafasi kujulikana, kwa nini ungependa kuwa maarufu? Kwa mfano, ujifanye kwamba ungeweza kufanya kitu chochote vizuri sana, na tafadhali usiseme ungekuwa kuwa mtaalamu mzuri, au ungefanya amani katika mahali pote, au kwamba ungewalisha watu wote. Bila shaka, vitu hivi ni muhimu, lakini ninapenda kufahamu tamaa nyingine zako kwa wewe mwenyewe tu. Je una heba za siri ambazo ungependa kuendeleza? Utuambie! Ukumbuke, hutakuwa fani tu, utakuwa mashuhuri sana. Nakutakia ujibu tofauti na majibu yaliyopita kuhusu pendekezo la utotoni na shughuli nyingine. Watu wengi watakufahamu, na namna ya washabiki wako itategemea juu ya sababu ya umashuhuri wako. Kwa hivyo, kwa nini kila mtu atajua jina lako?

Na Hilary

Msamiati:
ku*julikana -to be famous, in the limelight
maarufu -distinguished, famous
mtaalamu -scholar
heba -talents
fani -successful
mashuhuri -renouned, celebrated, illustrious
shughuli -career
umahuhuri -fame

Monday, May 4, 2009

Kumbukumbu ya Utotoni

Watu wote wana kumbukumbu nyingi kuhusu utoto wao, labda kuhusu likizo ya familia yao, au kuhusu shule ya msingi, au hata ndugu zao. Je, ni kumbukumbu gani uliyonayo kuhusu utoto wako unayoipenda zaidi? Ulikuwa mtoto mdogo wa umri gani? Ulikuwa mtoto mzuri, au mbaya? Ulifurahisha sana, au ulitasliti? Tueleze kuhusu utoto wako, tafadhali!

ku*tasliti - to stir up trouble

By Michelle.

Friday, April 24, 2009

Unazitumiaje pesa zako?

Ninapopata pesa kidogo, kwa kawaida huzitumia kuwa na tajariba nzuri. Kwa mfano, hula pale hotelini tamu au husafiri katika nchi tofauti. Watu wananiambia kwamba nilinde pesa zangu kwa ajili ya wakati ujao ama ninunue nguo au vitu vingine. Je, unapopata pesa, huzilinda au huzitumia? Ukitumia pesa, unapendelea kununua vitu au kuzitumia kwa ajili ya tajariba maalum?

Na Lisa.

Tuesday, April 14, 2009

Sikukuu unayoipenda.

Kesho ni siku ya mwisho wa sikukuu ya Passover. Unapendalea sikukuu gani? Una dini? Ungeweza kutengeneza sikukuu, ungefanya nini?

Sunday, April 5, 2009

Mipango ya maisha

Ulipokuwa mdogo, ulikuwa ukifikiri kwamba ungefanya nini utakapokuwa mtu mzima? Kwa nini ulipenda kazi hii? Mara kwa mara, nilifurahia kukumbuka mipango yangu kutoka utoto, kwa sababa yananichekesha. Kwa mfano, pengine, nilitaka kuwa daktari ya macho. Nilihitaji degaga nilipokuwa mdogo sana, na kapenda lenzi ambaye wao hutumia kuangalia macho. Pengine, nilitaka kuendesha ndege. Nilijua majina ya kila ndege (nimeyasahau sasa) na kaangalia katika mbingu kuziona kila siku. Pengine nilitaka kuwa mwandishi pia. Nilikuwa nikiandika hadithi fupi kuhusu familia kubwa inayekaa katika jimbo la Texas (ingawa sijawahienda Texas)! Labda ndoto hii ni karibu na nususi, kwa sababu ninapaswa kuandika kitabu ili kupata shahada ya tatu. Nimefurahi kwamba sikusomo udaktari wa macho au jinsi kuendesha ndege. Vitu hivi vingenichokesha sana leo! Je, mipango yako yamebadilika tangu utoto? Ulipenda kufikiri kuhusu wakati ujao au hapana?

Msamiati:
degaga (9/10) eyeglasses
lenzi (9/10) lenses
mbingu (9/10) sky, heavens
nususi (9/10) fact, reality

Friday, February 27, 2009

Vyakula Unavyopendelea

Sijui kuhusu ninyi, lakini mimi ninapenda chakula SANA. Ninahitaji chakula kula, bila shaka, lakini ninafurahia pia kuonja vyakula vya ajabu na kujaribu vyakula vipya. Ninapotafuta ladha ambayo sijawahi kula, ninajisikia kama kinywa kinakuwa hodari zaidi. Kwa mfano, leo usiku nilikula chokoleti na nyama ya nguruwe—nilishangaa, lakini ni tamu sana!

Hebu tuambie kuhusu vyakula unavyopendelea. Kuna chakula kimoja usingewahi
kutupa? Je ungeweza kula mlo umoja kwa maisha yote, ungekuwa kula nini? Tunda gani unapendelea? Na mboga gani? Nini chakula cha ajabu kuliko vyote ambavyo umekula? Ujibu maswali haya au utuambie hadithi nyingine kuhusu chakula. (Na tafadhali, uhakikishe huna njaa unapoandika au utahuzunika!)

Thursday, February 5, 2009

Kitabu cha burudani unachopendelea kukisoma.

Ukisoma Chuo Kikuu cha Stanford, unahitaji kupenda kusoma vitabu. Lakini, wanafunzi wa Stanford hawana saa ya kutosha kusoma vitabu kwa burudani. Je, kitabu gani cha burudani unapendelea zaidi? Ukipata wasaa, kitabu gani unataka kusoma badaaye?

Monday, February 2, 2009

Habari kutoka magazetini

Baada ya kusoma makala ya wiki hii kutoka IPP media umeona ni jinsi gani Rais Jakaya Kikwete amefanikiwa katika kusuluhisha migogoro iliyojitokeza katika nchi jirani mfano Kenya. Toa migogoro miwili amabayo ipo /imeshatokea katika jamiii yako na namna ya kuitatua.

Saturday, January 31, 2009

Mipango ya Kiangazi kijacho

Kwa kawaida, wakati wa mwezi wa pili, wanafunzi huanza kufikiri kuhusu kiangazi kijacho. Kwani hatuna madarasa wala pesa, na tunahitaji kuendelea na utafiti wetu, na kupanga mapema. Je, ungependa kufanya nini ? Kwa nini unataka kusoma Kiswahili wakati wa kiangazi au sasa? Na je ni kwa vipi utatumia lugha hii? Tafadhali, eleza kuhusu mipango yako.

Saturday, January 24, 2009

Maisha Tofauti

Wakati mwingine nikiwaza kuhusu maisha yangu yanavyoendelea ninaona kwamba ni bora kama nisingalisoma historia ya Afrika Mashariki katika Chuo Kikuu cha Stanford na kwamba ningalikuwa msanii. Je mngalibadilisha maisha yenu mngalifanya nini? Je, mngalisoma Chuo Kikuu cha Stanford? Mngaliishii hapa nchini Marekani au katika nchi nyingine? Mngalifanya kazi nyingine? Tafadhali wazeni kuhusu maisha yenu. Je mngalichagua njia / mpango mwingine wa maisha tofauti na wa sasa?

Sunday, January 11, 2009

Tofauti kati ya biashara za zamani na za sasa baina ya Afrika ya Mashariki na sehemu za dunia nyingine

Kumekuwa na biashara kati ya watu wa Afrika ya Mashariki na sehemu za dunia nyingine (kama Arabian Peninsula au Southeast Asia) kwa miaka mingi. Je kuna tofauti gani kati ya ufanyaji wa biashara wa wakati huu na ule wa wakati uliopita (miaka mia moja iliyopita, kwa mfano).